Saturday, March 17, 2012

Mambo ya Kuzingatia Katika Mapenzi

Uaminifu:
Katika maisha ya uhusiano, mpaka mnaamua kuwa wawili ina maana mmekubali kwa ridhaa yenu. Mmewaacha wengi na kuamua kuwa pamoja, hivyo mnatakiwa kulilinda penzi lenu kwa kuwa waaminifu.

Tabia nzuri:
Hii ndiyo inayobeba uwakilishi wa mwanadamu ndani ya nyumba, ndiyo nguzo imara ambayo itakufanya usimame popote kwa kujiamini.
Katika hili wengi hukosea wanapojiona wana sura na umbile zuri au fedha, basi huanza kuwanyanyasa wenzao kwa kujivunia walivyonavyo na kusahau hakuna kiumbe kilichoumbwa kwa ajili ya kukasirishwa.
Mara nyingi uhusiano wa watu huvunjika kutokana na tabia ya mmoja kuwa mbaya isiyovumilika.

Huruma:
Ndani ya uhusiano, huruma ni kitu muhimu sana, ukiwa nao, huwezi kumuumiza mwenzako.
Nyumba yenye huruma kwa wapendanao hudumu milele na kutenganishwa na kifo. Asiyekuwa na huruma, hufanya jambo lolote bila kujali maumivu ya mwenzake.

Upendo:
Huu ndiyo unaobeba kila kitu kwa vile mwenye upendo ana huruma, ni mvumilivu na tabia njema ndiyo asili yake. Wote mkiwa na upendo hata familia yenu itakuwa yenye tabia nzuri.
Hapa mara nyingi kumekuwa na tatizo kwa baadhi ya watu kuchagua watu hasa wanawake kuchukia ndugu wa mume na mwisho wa siku ndoa huvunjika.

Uvumilivu:
Huu ndiyo muhimu katika maisha yetu ya kila siku, wengi wasio wavumilivu, wamekuwa wakitengana na wenzao. Kuna vitu ambavyo tunatakiwa tuvumiliane kwa vile wanadamu ni viumbe wenye upungufu.
Kukosana ni sehemu ya maisha, lazima mvumiliane, mtangulize kusameheana na kuyasahau yaliyopita. Yapo ya kuvumilia, lakini si yaliyovuka mipaka kwa mtu kushindwa kujirekebisha.

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment