Monday, March 30, 2009

Hivi siku ya kwanza inauma

Hivi siku ya kwanza inauma?


"Nina miaka 21, ila bado ni bikra. Niina mchumba na tunapendana sana na tumekuwa pamoja kwenye uhusiano kwa mwaka mmoja sasa. Ananitaka tufanye ngono lakini mimi huwa naogopa sio tu kwa vile bado naishi na wazazi wangu bali pia rafiki zangu wananiambia Siku ya kwanza unaumwa sana mpaka unashindwa kutembea. Hii ni kweli? "

Jawabu: Ni kweli kabisa kuwa Siku ya kwanza kuanza ngono au siku ya kuondoa Bikira huwa kuna maumivu ambayo hutofautiana kutegemeana na mwanamke mwenyewe na mtindo wa maisha aliyo/anayoendesha.


Vilevile maumivu hayo hayo yanaweza kuwa sivyo kama inavyosemekana kwani inategemea zaidi na ufanyaji wa mpenzi wako, mapenzi yake kwako, uvumilivu, hali ya kujali na uelevu wa hali ya juu.

Kitu muhimu cha kuzingatia Siku ya kwanza ni kuwa-relaxed, kufanya maandalizi ya kutosha (romance) nakufikiria zaidi mapenzi yako juu ya mpenzi wako, utakapokuwa unasikia maumivu basi mwambie mpenzi wako asiingie na badala yake abaki pale alipo.....yeye kama mwanaume (kama ni mzoefu) ataendela kukupa denda kukushika au kukunyonya chuchu ili kukusaidia kunyegeka zaidi na vilevile uwe-relaxed.

Lakini kama unahisi huwezi kuvumilia mwambie tu kuwa mjaribu siku nyingine kwani sio lazima "utandu" utolewe siku moja inaweza kutoka ndani ya siku tatu au wiki (nikiwa na maana uume kuingia wote ukeni).


Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa Mpenzi wako ndio anataka kukungonoa (ni kawaida ya wanaume) hali inayokufanya na wewe ushawishike na kufuata mkondo, ili kuepuka kujilaumu ni vema basi kufanya maamuzi wewe mwenyewe, yaani amua kuwa sasa unadhani kuwa ni wakati muafaka wa kuanza kungonoka.

Inafurahisha kufahamu kuwa wewe na mpenzi wako mmechumbiana na ktk miezi michache mnakwenda kufunga ndoa. Ikiwa mpenzi wako na wewe mmeweza kuvumilia kwa muda wa mwaka mmoja ni wazi kuwa mnaweza kuvumilia zaidi mpaka mtakapofunga ndoa.

Mimi binafsi ningekushauri usubiri mpaka utakapofunga ndoa so long as mmechumbiana (kajitambulisha kwako na yuko tayari kukuoa) ili iwe "extra special" na vilevile kuepuka suala zimala kujilaumu ikiwa utaamua kufanya na "mchumba" alafu baada ya kumpa asikuoe.

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment