Friday, March 27, 2009

Kwenda nje ya Ndoa/Uhusiano/ukware/Umalaya

Kwenda nje ya Ndoa/Uhusiano/ukware/Umalaya

Kwa maana ya haraka haraka ni mtu asiye na adabu/heshima, huruma, utu, muharibifu, mkatili, mlafi, mshamba na ni muuaji vilevile.

Tatizo hili limekithiri katika jamii yetu na sasa limekuwa ni jambo la kawaida kwa baadhi ya watu au kwa maana nyingine wamefanya kuwa ni utamaduni wa kisasa (kwenda na wakati).

Tabia hii mbaya huathiri kwa kiasi kikubwa baadhi ya familia hasa ikiwa muhusika yuko ndani ya ndoa na amefanikiwa kupata Watoto.

Tabia hii haiko ndani ya ndoa pekee bali hata katika mahusiano ya kawaida ya kimapenzi tofauti ni kuwa ndani ya ndoa akina Baba ndio wako mstari wa mbele na walio nje ya ndoa baadhi hulipiziana visasi.

Wanawake walio katika ndoa hujitahidi kuwa wavumilivu wakiamini kuwa ndoa ni uvumilivu. Hapana! ndoa ni kuvumiliana (wote wawili) ikiwa mmoja wenu ana matatizo kiuchumi, kuugua, ajali n.k, lakini sio kwenye Uasherati...

Baadhi ya wanawake hushindwa kufanya uamuzi hasa ikiwa mwanaume ndiye “kitega uchumi” au wanafuata maadili mema. Wengine hung’ang’ania kubaki katika ndoa “for the sake of kids” na hii ni kutokana na kutokuwa na kipato kitakachomfanya amudu maisha yake na watoto ikiwa ataomba/kupewa Talaka.

Pamoja na mambo au sababu nyingine zinazopelekea tabia hii mbaya hizi zifuatazo hupelekea watu kutoka nje ya uhusiano wao wa kimapenzi/ndoa.

*Kutopata mapenzi ya kweli hasa ikiwa Kijana/Binti alilazimishwa kuoa/kuolewa na mtu ambaye hakumpenda “for the sake of Radhi ya Wazazi”, maadili, kuhofia umri n.k..

*Uchafu, kutojijali au kujipenda.-Wote mwanaumena mwanake.

*Kutoridhika au kutosheka na wakati mwingine uroho tu- Wanaume zaidi.

*Mmoja wenu kuwa na shughuli nyingi za kikazi/Biashara, kusafiri – Wote mwanamke na mwanaume..

*Tamaa ya kumiliki vitu Fulani –Wanawake zaidi.

*Kujaribu na kujifunza mambo mapya/mitindo lakini kutokana kufuata maadili unaogopa kuwa wazi kwa mpenzi wako-Wake kwa waume..

*Kukosa tendo la ndoa kwa muda mrefu ikiwa mwanamke ana Mimba kubwa /amejifungua n.k-Wanaume.

Pamoja na mambo mengine mapenzi ni kuambizana ukweli, ikiwa mwenzi wako hakuridhishi, mchafu n.k ni vyema ukatafuta muda na ukamweleza taratibu tena kwa upendo, kumbuka hakuna Mwanadamu aliyekamilika hapa Duniani kila mmoja ana kasoro zake.

Mpenzi wako (haijalishi mwanaume/mwanamke) ni kama mtoto anatakiwa kubembelezwa, kuelekezwa na ikiwezekana kufundishwa baadhi ya mambo ambayo hayajui.

Sababu za Kusaliti Pendo

Dalili kuwa mpenzi anatereza

Dalili za Uhusiano Unaoharibika

Yale yanayoweza kuharibu ndoa!

penzi ni nini hasa

Misingi ya Uhusiano wa Kimapenzi

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment