Friday, March 27, 2009

Maambukizo ya HPV

Maambukizo ya HPV

Human Papilloma Virus (HPV) ni maambukizo yanayotokea sana wanawake na huambukizwa kwa kufanya ngono, unapata maambukizo haya hata ukitumia kinga (Condom). Baadhi ya maambukizo haya huweza kusababisha Saratani iitwayo "Cervical" au Saratani ya Kizazi ambayo inaweza kusababisha usiweze kushika mimba/zaa ktk maisha yako yote au maambukizo mengine huko ukeni ambayo sio yale ya Ngono tunayoyajua nakutajia kila siku.

Hakuna dalili zozote za Saratani hii ya kizazi lakini ukiwahi kujua kuwa unayo kwa kufanya kipimo kiitwacho "Smear" basi unakuwa umeokoa maisha yako kwani Saratani hii inaua wanawake sambamba na ile ya Matiti.

Mwanamke anaeanza ngono mapema (chini ya miaka 21) anakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata Saratani hii na wale wanaoanza Ngono ndani ya miaka 20 huwa x2 kwenye hatari ya kupata Saratani hii.

Tumia Condom

Mpenzi wangu hataki kuvaa kondomu

Kutumia kondom ya wanawake

Kutumia kondom ya wanaume

HIV na Ukimwi barani Afrika

Ngono Salama


Mapenzi salama

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment