Friday, March 27, 2009

Penzi halilazimishwi

Penzi halilazimishwi!



Natambua kuwa kila mtu ana tafsiri yake ya neno mapenzi au maana halisi ya kupenda. Moyo wako siku zote unajua pale unapompenda mtu na hivyo huhitaji kuulazimisha, kuushawishi au kuomba ushauri kwa watu wengine kama itakuwa sahihi kuwa na fulani au la!

Penzi na jinsi linavyojitokeza ni hadithi ndefu na inachanganya, sote tunajua swala zima la mapenzi linachanganya na halina kanuni lakini ni moyo wako pekee ndio utakao jua kama hapo "umefika bei" au la!


*Penzi tamu na mara nyingi hudumu kwa muda mrefu ni lile lililo na chanzo kwenye urafiki. Urafiki mwema siku zote huwa hauna mwisho hali kadhalika mapenzi ya kweli hayana mwisho sasa hebu changanga pamoja uone matokeo.

Mnapokuwa marafiki kwanza nakuzoeana sana kiasi kwamba mnasaidiana vilevile mnakuwa huru au wazi ktk kuzungumzia mambo binafsi kama vile furaha, matatizo,mafanikio namengine mengi muhimu napengine kujua mapungufu yenu ambayo kama marafiki mnakuwa tayari mnajua jinsi ya kuishi nayo aukuyavumilia na hivyo mnaendelea na maisha yenu yenye furaha na amani kama marafiki na wakato huohuo wapenzi.


Tatizo la penzi lililojengeka ktk urafiki ni kwa mmoja wenu kuhofia urafiki kufa ikiwa ataziweka hisia zake wazi kwa mwenzie. Ikiwa utamkataa ni wazi kuwa itakuwa ngumu sana kwake kuvumilia kukuona wewe kuwa na mtu mwingine kama mpenzi na sio yeye.


*Penzi liloegemea kwenye kupendeza/kuvutia hufa au hufikia kikomo mara tu mmoja wenu anapobadilika au kutovutia tena kutokana na sababu tofauti za kimaisha. Ukitaka penzi libaki pale pale basi ni wajibu wako kuendelea kuwa hivyo ulivyo (kupendeza/kuvutia).


Nakumbuka juzi nikiwa kwenye “office” , Jamaa (nafanya nae kazi) akinilalamikia kuwa “My wife didn’t look like that when we met, she was so hot like those women” (akionyesha wanawake wenye maumbile mazuri na wamependeza kimavazi)” nikamuangaliaaaaa kisha nikamuuliza unadhani hakuvutii tena?


Akasema “ndio, hata kufanya mapenzi inakuwa ngumu siku hizi”. Nikamuuliza tena huoni kuwa amekuwa hivyo alivyo kwa sababu yako? Akauliza “kwanini” nikamwambia hukumwambia wazi kuwa unachopenda kwake ni “the way she look, nothing more” angejua angefanya uamuzi wa busara kuliko kufunga ndoa na wewe na kisha kukuzaliya watoto. Nikamwambia the woman needed/needs ur love and support!........

Penzi lisilo na mwisho ni lile linalijotokeza kiasilia (naturally) kwamba unakutana na mtu (sizungumzii love at 1st sight hapa) kisha mnajikuta mnapendana kwa dhati penzi hili hunawiri vizuri sana na hudumu kwa muda mrefu na ikitokea mmoja kumuacha mwenzie basi itakuwa ni sababu “nzito” ambayo ni kifo (ndio pekee kitatenganisha penzi hili).


Atakae baki humuia vigumu sana kuwa na mpenzi mwingine na itamchukua muda mrefu sana “kumdondokea” mtu mwingine “Bond” ya penzi hili ndio wengine huita penzi la kweli.


penzi ni nini hasa

Misingi ya Uhusiano wa Kimapenzi

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment