Tuesday, March 31, 2009

Mme Mchafu alafu anapenda Punyeto

Mme Mchafu alafu anapenda Punyeto


"Mimi ni mdada, mwenye miaka 30, pia nipo kwenye ndoa miaka 8. Kwa bahati mbaya nipo kwenye lile kundi wasiokuwa na watoto ila si tasa, nikiwa kwenye ndoa niliwahishika ujauzito ukafikisha miezi 8 ikaharibika na kufanyiwa upasuaji hadi leo hii sijabahatika tena.


Pia ingawa mume wangu yeye alishakuwa na watoto before hajanioa mimi namshukuru Mungu sipati manyanyaso yoyote ya suala la mtoto toka kwa mume wangu, daima anaamini siku mungu atashusha baraka zake.


Kama isemekavyo ndoa nyingi ndoana, kuna baadhi ya vidudu kwenye ndoa yangu vinanipa wakati mgumu sana, jamani msione wanandoa wanatoka nje ni wazi kuna kitu ndani, eeeehehe ile mada ya kusema "mume namtaka bf namtaka" ilinifurahisha, ingawa mimi bado sijafikia kutoka nje.

Tatizo la kwanza, ni mume wangu hupenda kupiga bomba sanaaa, yaani nyeto, mimi najiamini kwenye sita kwa sita naujua mchezo, nilipoanza kugundua hilo miaka mitano iliyopita. Kuna siku nikiwa sipo chumbani hujikamua mwenyewe, mara za kwanza nikawa mkali kwake nikimwambia ina maana mimi sikuridhishi?

Pia anapojua nina hasira naye huja juu kama moto wa kifuu. Any way si njia mbaya kujisaidia mwenyewe unapozidiwa ila tatizo linakuja pale mimi ninapotaka kutombana, jamani jogoo halisimami sawasawa nadhani ni kutokana alishapiga nyeto wakati nimetoka, sometimes anafanya kushikilia ndio aingize ila ni ngumu.


Tabia yake hii imeniathiri kwani huwa najiuliza sasa mtu wa hivi ukiwa na housegirl au ndugu wa kike kwenye nyumba je si anaweza kuwatomba kama umetoka?basi mimi housegirl si mwajiri, kwa sababu nina sevente coter ya mlinzi basi namlazimisha mlinzi awe na mkewe ili aweze nisaidia kazi za ndani pale ninaposhindwa, lakini nae kwa mashariti kuwa ukiona sijaamka marufuku kuingia kwangu, pia mpaka nikuite ndipo uje ufanye usafi.


Basi tabia yake hiyo inanifanya niumiee sana, na mimi ikafikia hatua najichua mwenyewe ila si enjoy sana kwani nahitaji denda, maromance, basi some time najiandaa mwenyewe kinyegenyege naandaa kitanda changu kwa mshambulizi nikijua leo kazi, basi mtoto wa kike natoa mapozi kitandani hata kama kuna baridi mimi najichanua nikijua namdip kumbe wapi!


Nimeshamueleza ten times bila kujirekebisha. Sometimes nimelala usiku mume wangu huamka kwenda computer kuangalia ma sex, na kujimaliza, nikitokea tu anashtuka anafunga program au hufungulia tv ya bedroom bila sauti anacheck kisha anaenda jimaliza.
Je jamani ndoa za namna hizi si vichochezo tu vya kusalitiana.


Tatizo la pili shost ni kuoga, mmh am so sorry kutoa siri za ma husband, yaani mimi ni mtoto wa Kitanga najua mapenzi, yaani yaweza pita siku 2 au 3 bila usafi wake wa mwili, na tuna warm shower muda wote, so sometime unajisikia kumshukia mume wako wakuta harufu za ajabu ajabu, sasa ukiwa pale unakula koni kidizaini jamaa anakukandamiza kichwa ili uende chini, yeye hajui kama nanyonya kwa pozi. Raha ya mapenzi usafi bwana hapo mtarambana mpendavyo, hata hili nimejaribu kumshauri bila mafanikio.


Lingine ndugu zanguni, mume wangu hataki mimi nijishughulishe na kazi yeyote ya kuniingizia kipato. Kila ukimwambia ooh mimi nina mshahara wa kututosha, pesa inatosha. Ila ukitaka labda ka' milioni ni for what, why, nalo hili limenichosha kuwa goli kipa tu. Samahani kwa mambo mengi ila naombeni ushauri, naogopa nikitoka kwa huyu nami uzazi wa matatizo, ni mwanaume gani tena atanivumilia."

Jawabu: Asante Dada,Kwenye maelezo yako umegusia suala la uchafu, huenda ndio sababu kuu ya yeye kujitenga au kukutenga kama sio wewe kumtenga na kumpa "mchezo" usioridhisha kwa vile huwezi kuvumilia harufu mbaya ya mwili wake.


Tatizo la kwanza; yeye kupenda kujipa mkono tena mbele yako ni kitu kizuri na ulipaswa kum-join badala ya kuwa mkali. Kujua kwako mchezo sio sababu tosha ya yeye kutojisaidia mwenyewe......huenda unaujua mchezo lakini humridhishi kwamba unayomfanyia yote hayamfikishi ila kumpa mkono.


Ni vema kuwa uligundua hili miaka mitano iliyopita, huenda aliibua au kurudia tabia yake pale ulipokuwa kwenye wakati mgumu baada yakupoteza mtoto (mimba), unapopoteza "mtoto" kwa kawaida wewe mwanamke unaweza kuathirika kisaikolojia na ukabadilika kabisa bila wewe mwenyewe kujigundua.


Inawezekana mume wako aligundua hilo lakini hakutaka kulalamika au ku-demand ngono kwa vile alikuwa anakuonea huruma...alikuwa more understanding kutokana na hali halisi uliyokuwa nayo na wakati mgumu uliokuwa nao na huenda yale mabadiliko wewe hukuyaona.


Kupenda kwake kujipa mkono hakuna uhusiano wowote na "umalaya" hivyo ondoa kabisa suala la yeye kutembea na msichana wa kazi au hata mwanamke mwingine yeyote nje ya uhusiano wenu. Huyu bwana anapenda na anahisi kuridhika zaidi akijipa mkono na si vinginevyo.


Hata kama ungekuwa wewe Mdogo wangu kama kuchezewa kisimi ndio kunakupa raha zaidi ya "full" ngono alafu mumeo hataki kukupa au hataki ufanye hivyo lazima utamwendea juu.....usicheze na utamu wa mtu aisee! Hakika mara baada ya kujipa mkono halika kusimamisha tena itamchukua muda kama sio siku (inategemea na jinsi gani alivyozoea na vipi ana-enjoy punyeto).


Kumuambia bila kuingiza vitendo na kubadilisha mfumo wako wa ufanyaji mapenzi na kumridhisha mumeo haisaidii, kitendo cha wewe ku-give up ndio kosa na ndio maana anaibukia kwenye "porn" ili kunyegeka kabla yajajipa mkono....


Tatizo la pili;Tatizo la watoto wa Kitanga mnapenda kuonjesha ili mwanaume atangaze ndoa au abaki na wewe milele (asikuache) baada ya Njemba kuotesha miziz mnabaki kujipa sifa za kumwaga kuwa mnajua mapenzi lakini mnasahau wajibu wenu kuwa mapenzi na mashamu-shamu huwa hayana mwisho na matokeo yake ndio hayo.....Mfano ulimzoesha kumuogesha, kumbeba, kumfukiza sijui mizizi gani, kumpala na kufanya nini sijui kitanga, zee la watu likazoea na matokea yako hata kujiswafi mwenyewe aona taabu.


Suala la msingi au niseme muhimu kwenye uhusiano wa kimapenzi sio "Utoto wa Tanga" au kuyajua mapenzi (unaweza ukadhani kuwa unajua mapenzi lakini kumbe kwake hujui kitu au humridhishi) bali ni kujua nini unaweza ku-offer kwenye uhusiano wenu. Ikiwa wewe mtoto wa Kitanga ulidhamilia ku-offer mapenzi ya Kitanga na ukaanza na "speed" hiyo mwanzo ulipaswa kutoipunguza no matter how mchovu you are!


Wanawake wengi huwa hawajui kuwa unapomzoesha mwanaume jambo mwanzoni kabisa mwa uhusiano huwa anategemea au anataka hayo yote yaendelee kuwepo kwa maisha yake yote atakayokuwa na wewe. Lakini kwa vile wengi huanza na ile "full speed" mara baada ya uhusiano kukomaa unajikuta umejichokea na matokeo yake mume/mpenzi anatafuta namna nyingine ya kupata masham-sham.


Ndio maana ukitaka kuwa na mume ambae atakuwa nakusaidia vijishughuli ndani ya nyumba unapaswa kumzoesha tangu awali kabisa mnapoanza uhusino(kabla ya ndoa).


Mf-Unapokwenda jikoni kupika, muite mpenzio na umwambie kuwa unapenda kampani yake au hata kuongea nae wakati unaendelea na kupika, kuwa kwake pale kutamfanya yeye kushika kisu na kukata kitunguu au hata kuweka vyombo kabatini kama sio kukupa chumvi n.k


Lakini ikiwa kila unapofanya shughuli unamuacha anatazama TV au anachat kwenye PC ndugu yangu mkija funga ndoa utaiona nyumba chungu, hasa kama wewe ni mwanamke unaefanya kazi.


Tatizo lingine; Kama nilivyosema hapo awali, mumeo kazoea "utanga" na huenda alikuoa akijua hutokuwa mtoka nje ili watu wengine wakuone. Wanawake wa Kitanga nasikia ni watu wa kujipara na kukaa ndani kumsubiri bwana arejee ili umpe mapenzi ya Kitanga....sasa leo hii ukurupuke kwenda kufanya kazi ndugu yangu si wataka Talaka weye!


Yote kwa yote, Mumeo anahitaji serious talk na wewe, kaa nae chini na zungumza nae, lazima kule Tanga wakati unafundishwa namna ya kumfurahisha pia ulifundishwa namna ya kumpenda kwa hali yeyote, namna ya kuzungumza nae kwa mapenzi ili kuwakilisha hoja yako, namna ya kumshawishi na kuikubali hoja yako, namna ya kumfanya afanye yale utakao wewe (kukushirikisha anapojipa mkono, kuacha kukimbia kitandani na kwenda kwenye Porn, kuwa msafi) na si vinginevyo......that is what we call "kujua mapenzi".....kuyajua mapenzi is more than ufikiriavyo Mdogo wangu.


Rudi nyuma, kumbuka ulivyofundwa na kila kitu kitakuwa safii na utafurahia maisha yako ya kimapenzi, ngono na mumeo.

Usafi na Ngono


Kupiga Nyeto kwa Wanawake

Punyeto

Uwazi katika ngono

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment