Tuesday, March 31, 2009

Nenda taratibu lakini changamka katika mapenzi

Nenda taratibu lakini changamka katika mapenzi!


Mara nyingi wanawake huwa anapenda au kutaka kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na kila kitu kiende sawia kabisa bila matatizo, hii ni kutokana na sababu nyingi tofauti kama vile

-kuwa mpweke kwa muda mrefu,
-kuwa na "foleni"ndefu ya mahusiano mafupi na sasa anahisi kuwa wakati umefika wa kukaa na kutulia na mtu mmoja,
-uoga wa kuachwa/kuumizwa,
-kuhisi ameachwa(left out) kwa vile rafiki zake wana wapenzi,
-kuhisi umri umekwenda n.k.


Haijalishi una uzoefu mbaya au mzuri ktk mahusiano ya kimapenzi…unachotakiwa kufanya ni kutuliza akili na kucheza taratibu. Ukichukulia mambo taratibu itakusaidia sana kujua hisia zako juu ya mwenzio na pia kumjua/fahamu huyo mpenzi kabla mambo hayajawa “makini” hali itakayokusaidia kutoumia sana ikiwa atagundua kuwa humfai au wewe kutambua kuwa hayuko vile ulivyotegemea n.k.


Vilevile kwenda kwako taratibu kutamfanya huyo “mpenzi mpya” kuwa “comfortable” na wewe, kwa vile hautokuwa mtu wa kulazimisha mambo yatokee vile unavyotaka……..wanaume wengi hawapendi kuwa “pushed” kwa vile uhisi hawapendwi bali unapenda kufanikisha jambo fulani kama ktk maisha yako na sio kwenye maisha yenu “as a couple”.


Kumbuka kuwa wanaume hutumia uongo mwingi ili “washinde” na wakupate, hivyo kuwa mwangalifu najifunze “kuchuja” maneno/mistari yao wanapokushawishi/tongoza uwe nao, mara nyingi hutoa ahadi nyingi ambazo hu-“sound” kama wanaji-“commit” kwako kabla hata hujawajua vema.


Wewe kama mwanamke unatakiwa kuwa makini, msikivu, mwelevu na mwepesi kuhoji ikiwa utahisi unayoambiwa ni “too much….too soon”, sio macho chini na kila kitu….Ok, haya, sawa, ai wewe……ndio…..wasema kweli mjuba…..n.k.……changamka!


Kumbuka kitakacho kufanya umdondokee mtu kimapenzi kabla hata ya kungonoana sio muonekano wake tu (au pesa kwa wengine wazembe-wazembe) bali kumjua kiundani baada ya kuzungumza nae……unapomhoji mwenzio ni rahisi kujua uta-offer nini kwenye uhisiano ili uwe bora na yeye atachangia vipi ili mtoke “pea” nzuri na ya muda mrefu.


Maelezo yake kutokana na maswali yako yatakuwezesha wewe utafakari na kufanya uamuzi wa busara hali kadhalika maswali yako yatamfanya yeye afikiri zaidi ikiwa ni myeyushaji/muongo lakini “anakutaka” basi anaweza kubadili yote aliyosema/ahidi jana kwani kagundua kuwa wewe sio wa kudanganyika…..na akiendelea hamtofika mbali….hii yote nitakuwa imetokana na kuchangamka kwako kwenye kuhoji pale ulipohisi jamaa natoa ahadi kamavile ninyi ni “couple” tayari kumbe ndio kwanza mna-date.


Kumbuka mtu anapoku-“date” haina maana kuwa mko kwenye uhusiano na mara nyingi hushauriwi kufanya ngono ktk kipindi hicho……”date” inaweza kuchukua siku tatu mpaka miezi 4 kabla hujajitolea mwili wako.

penzi ni nini hasa

Misingi ya Uhusiano wa Kimapenzi

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment