Tuesday, March 31, 2009

Ombi lake la T-O laweza kuua uchumba wetu

Ombi lake la T-O laweza kuua uchumba wetu

Ngono kinyume na maumbile

Uwazi katika ngono

"
Mimi nina mchumba wangu ambaye natarajia kufunga ndoa naye hivi karibuni. Tumekuwa katika uchumba kwa miaka miwili hivi, na sasa tuko karibu ukingoni mwa safari yetu ya uchumba na kuingia katika ndoa.

Tatizo likakuja pale huyu mwenzangu tunapokuwa kwenye ile raha ya kurushana(kutombana) huwa tunafurahiana sana, lakini huyu mwenzangu amekuwa akinisumbua sana na jambo moja ambalo limekuwa kero sana masikioni mwangu na kuniletea kinyaa.

Kwa mara ya kwanza tulipokuwa tunatombana na mchezo umenoga, nilisikia mwenzangu akisema tafadhali naomba unitombe kinyume na maumbile, Yaani kwenye mkundu eti nasikia ni kutamu sana na kwenyewe tujaribu. Mimi nilimkatalia na kumwambia siwezi kufanya kitu cha namna hiyo.Na nilimwambia tena naona kinyaa kabisa hata kusikia hivyo.Akanielewa yakaisha.


Safari ya pili baada ya kupita muda kiasi tukiwa katika mchezo huohuo akawa kanogewa mno tena akaniomba akisema naomba tujaribu tu kwani hatutakuwa tunafanya hivyo kila wakati. Nikasema naomba sana unielewe kwamba huo mchezo nauchukia kama ugonjwa wa ukoma na pengine zaidi ya hapo. Akaomba radhi kuwa amekosa.


Mara ya tatu ambayo ni kama wiki moja limepita na ni miezi sita imepita tangu aliponiomba mara ya pili, nikashtukia tena ananibapa kwa upole, na kwa utaratibu tukiwa kwenye utamu huo, akaanza tena akisema lile jambo kama inawezekana kujaribu tu kwani amesikia mara nyingi kwamba ni kamchezo katamu, hebu tujaribu tu.

Mimi hapo niliona sasa huyu bila shaka amewahi kufanya kamchezo hako, ikabidi nimuulize nani alimwabia au je, uliwahi kufanya?Akasema huwa anasikia tu katika story hasa akiwa chuoni na katika mazungumzo ya kawaida.

Pia alisema yeye hajawahi kufanya, ingawa aliwahi kufanya ngono na mtu mwingine kabla ya kukutana na mimi lakini kwa njia ya kawaida. Ila yeye amesoma digrii yake nchini Marekani sijui huko ndo kapata hizo story au vipi. Basi mimi nilimkatalia nikamwambia muonja sukari huvyonza yote maana yake huo utakuwa mchezo wako wa kila siku na usipoupata hapa ndani utautafuta nje. Na nikasema nachukia mno kusikia kitendo hicho.Basi akaachia hapo.

Yeye anafanya kazi Morogoro na mimi nipo Dar.Huwa tunakutana kila wiki anaweza kuja kwangu au nikaenda kwake.

Tafadhali nisaidie ni namna gani nimasadieni huyu mchumba wangu ili jambo hilo limtoke mawazoni mwake na pia aweze kunielewa jinsi jambo hilo linavyonikera, hasa akiwa ni mama ninayemtegemea kujenga familia pamoja nami.

Maana nadhani atalirudia tena kulihitaji, na labda hapo inaweza kuwa mwisho wa uchumba maana jambo hilo linaniudhi kupita kiasi. Kwa kweli tunapendana na tena ni mdada mwenye sifa zote za umama na mwenye urafiki na upendo kwa watu wote, hasa ndugu zetu. Lakini hilo ombi lake jamani linanipa hasira mimi."

Jawabu: Asante sana kwa kuniandikia, Natambua kuwa sisi wanadamu huwa tunafanya zaidi yale mambo ambayo tunakatazwa au tunaambiwa ni mabaya, kutokana na Imani zetu za Dini kuzini ni kubaya au ni Dhambi lakini wangapi tunafanya ngono kabla ya ndoa?


Tunaambiwa kuwa ngono bila Condom inahatarisha maisha yako kwani unaweza kupata VVU, tunaona waliovipata na wanaindoka lakini wangapi wanatumia "ndomu" kila wanapofanya ngono? T-O ni mbaya na ina madhara makubwa sana kwa mwanamke ikiwa inafanywa mara kwa mara na kusababisha ulegevu kule nyuma, lakini watu wanatigoliwa kama hakuna uke vile.....!

Ngono inafanywa au niseme inafanyika ktk mikao na mitindo mingi tofauti, mitindo yote hiyo tulikuwa hatujui raha yake mpaka pale tunapojaribu na kugundua ala! kumbe hii inaongeza "stimu" au raha ya kufanya mnachokifanya.


Sio wakati wote mtu anapokuja na jambo nakuomba mjaribu au kufanya inamaana kuwa tayari kaisha lijaribu kabla......hapana! Kama ilivyo kwenye suala zima la kuanza kufanya ngono, unapoomba mpenzi akunyonye uume/uke au hata akubusu kwa mate (denda) haina maana kuwa huyo muombaji tayari alishawahi kuliwa denda hapo awali.


Huenda amesikia tu kuwa kuna raha au ni tamu na sasa anapenda kujaribu na mpenzi wake ampendae, mpenzi ambae anamuamini, anajisikia nae huru kufanya na kujaribu chochote, hii ndio faida ya kuwa muwazi kwenye uhusiano.


Binaadamu tunafurahi ngono kwa namna tofauti, kuna wale wanapenda kutukaniwa wazazi wao wakati wakifanya mapenzi, wapo wanaofurahia kuliliwa, wachache wanapenda kupigwa au kufinywa/kung'atwa (maumivu) huku wanafanya, wengine wanapenda kutumbukizwa dole wanapokaribia kileleni, baadhi wanapenda kunyonywa matiti wakati anatiwa, vilevile kuna wengine wanapenda kusikia neno "nakutomba au tunatombana", pia kuna baadhi wanapenda kuambiwa (ahidiwa) kupewa mwezi, nyumba n.k......ilimradi mtu anafanyiwa au anasikia kile kinachomfanya afurahie zaidi kufanya ngono.


Inawezekana kabisa Mchumba wako aliwahi kujaribu na mpenzi wake wa zamani na sasa angependa kujaribu na wewe au kama ilivyo kwa wanawake wengi Bongo, anadhani kukupa tako ndio tiketi ya wewe kutangaza ndoa (hasa kama bado hujafanya hivyo) vilevile huenda anataka kukupa tako ili usijeenda kutafuta nje, kwa maana nyingine anakuambia ukihitaji "she is up for it".


Sio kweli kuwa mwanamke aliyewahi kutigoliwa mara kadhaa "O" yake inakuwa kubwa (natumaini unalijua hilo kutokana na kuujua mwili wa mchumba wako, lazima uliwahi kumpa dole huko nyuma), mkundu hutanuka (kupeteza marinda/misuli) ikiwa mhusika anafanya kitendo hicho mara kwa mara na wanaume wenye "viungo" vikubwa hali kadhalika matumizi ya SanamuNgono.


Kutokana na maelezo yako (huwa anakuja na issue ya "O" mnapofanya mapenzi), kitu kinachoashiria kuwa huenda anapenda kulitamka hilo neno, sasa kwa vile hupendi wewe huwa unakataa, inawezekana kabisa kule kukataa kwako ndio kunamuongezea "stimu" ya kuendelea na safari.....huwezi kusema hupendi kabla hujajaribu na kujua kama utapenda au hutopenda.....sema hutaki, na ofcoz takwa lako linapaswa kuheshimiwa.


Nini cha kufanya-Zungumza nae na muambie ukweli kuhusu T-O na madhara yake kabla hajakumbushia, mueleze unavyojisikia kutokana na tendo lenyewe kuwa kinyume na maumbile na vilevile ni kinyume na Imani za Dini (kama unaamini Dini), mueleze heshima uliyonayo kwake kama mwanamke na kamwe usingependa kufanya kitendo hicho kwa vile wewe unahisi kuwa ni udhalilishaji wa mwanamke kwa vile yeye mchumba wako ana Uke na unaupenda uke wake.


Mhakikishie jinsi gani unampenda yeye, namna gani unaupenda uke wake na kwamwe usingependa kufanya ngono kinyume na maumbile kwa vile ni kinyume na Imani yako ya Dini(kama unaamini) na unadhani ni kitendo cha kumdhalilisha mwanamke kwani tayari yeye (mchumba wako) ameumbwa na uke na unaupenda na kuridhika na uke wake huo.


Mwambie Mchumba wako kuwa ungependa na uko tayari kujifunza mbinu nyingine za kuridhishana kimapenzi na ungependa ushirikiano wake (hakikisha unamfanyia vitu vingine kama vile kumnyonya kisimi/uke, cheza na mwili wake kwa ustadi wa hali ya juu......nasikia sehemu kubwa ya wanaume wa Kiafrika hapa huwa ni mbinde...sijui ni uvivu au kutojali?)


Mchumba wako kama muelevu atatambua kuwa uko makini kuwa hutaki kufanya wala kujaribu kitendo hicho, hivyo kama ni "mke mwema" ataheshimu hilo na kuanzia siku hiyo hatokuomba tena umfanye matakoni, vingivenyo (akiendelea kuibuka na hoja yake ya T-O) basi muambie wazi na kwa mara ya mwisho kuwa kama kuingiziwa uume mkunduni ni muhimu sana kwake na anajua wewe hutaki na kamwe hutofanya hicho kitendo basi ni vema kila mtu achukue ustaarabu wake.

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment