KUJIAMINI ni hali ya kuwa na uhakika juu ya kile unachokifanya, tenda, nena na hata muonekano kwa ujumla.
Kujiamini kunasaidia sana katika kutafuta njia ya mafanikio maishani. Ni suala la muhimu sana kujiamini.
Mwandishi mmoja wa vitabu vya saikolojia, Ben Carson aliwahi kuandika;
‘Confidence can pull you to success’ (Kujiamini kunaweza kukusogeza palipo na mafanikio).
Kwa nini watu hawajiamini? Kutojiamini kunatokana na nini? Haya ni baadhin ya maswali ambayo ni lazima tujiulize.
Utamjuaje  mtu asiyejiamini? Hapa chini nitaainisha dalili tano za mtu  asiyejiamini kabisa. Lakini pia kabla sijaendelea mbele zaidi, naomba  niweke kumbukumbu sawa kuwa, mtu asiyejiamini ni nadra sana kufanikiwa  maishani.
KULALAMIKA
Dalili ya awali kabisa ya mtu  asiyejiamini ni pamoja na kulalamika kila mara. Yaani jambo dogo tu  lakini malalamiko yanakuwa mengi kupita jambo lenyewe.
Mwanasaikolojia  mmoja nchini Marekani, Willie Jollie katika kitabu chake cha It Only  Takes A minute to Change your Life, aliandika kuwa;
‘Too much  complaining proves how weak and unconfident you are’ (Kulalamika kupita  maelezo kunathibitisha ni kwa namna gani ulivyo dhaifu na hujiamini).
Mtu  wa kulalamika, anakuwa hawezi kujisimamia juu ya jambo f’lani pasipo  uwepo wa wengine na pia kulalamika sana kuonesha ni jinsi gani hujiamini  katika kufanikisha mambo maishani.
Lakini pia, kulalamika  kunaambatana na woga katika maisha kwani mara nyingi mtu muoga haishi  kulalamika hasa anapoachiwa jambo f’lani alitende peke yake. Hivyo  dalili ya awali kabisa ya mtu asiyejiamini ni pamoja na kuendekeza tabia  ya kulalamika kila wakati.
Mtu anayejiamani hapendi kulalamika, badala yake hutenda mambo kwa vitendo na si malalamiko.
Lakini  pia, tafiti za kisaikolojia zinaonesha kuwa, watu wanaopenda kulalamika  ni wale wenye maneno mengi ambao kazi yao kubwa ni kuongea na si  kutenda. Hili ni jambo baya sana maishani. Achana na maneno mengi,  jiepushe na tabia za kalalamika ovyo, fanya kazi kwa vitendo huku  ukitumia muda mwingi kuwa kimya.
KUTEGEMEA SANA WENGINE
Kuna  baadhi ya watu hawawezi kufanya jambo lolote maishani pasipo kutegemea  mawazo ya  wengine. Hata kama jambo hilo liko ndani ya uwezo wake lakini  hawezi kulitenda hadi atakapoambiwa na watu, sasa tenda.
Watu hawa  huwa na uwezo mkubwa sana ndani yao lakini hushindwa kujisimamia  wenyewe. Hata kama ana fedha kiasi gani, lakini hawezi kutenda jambo  bila kusukumwa.
Mfano utakuta mtu anataka kuchukua hatua fulani nzuri sana lakini anashindwa hadi baadhi ya watu wamuamulie ndipo atende.
Mfano  mtu amegombana na mkewe anakuwa hawezi kuamua nini cha kufanya juu ya  suala hilo na hapo ndipo atakimbilia kwa rafiki zake kuwaomba wamsaidie  nini cha kufanya jambo ambalo huashiria ni kiasi gani hajiamini.
Usiishi  kwa mawazo ya wengine. Hata wewe una akili kama wao na pengine  kuwashinda lakini unakuwa huna uhakika na unachokiwaza na kuona kama  bila wao huwezi kujisimamia maishani. Hii ni hatari sana. Jitegemee,  jiamini, tenda mambo kwa kutegemea muongozo wa upeo, busara, maarifa,  akili na mawazo yako mwenyewe. Ni suala la utulivu tu.
Thursday, March 15, 2012
Dalili 5 za Mtu asiyejiamini I
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment