SABA:  Namna nyingine ya kukabiliana na mawazo ya kuumiza ni kupunguza hasira  juu ya watu wengine. Katika hali ya kawaida matukio mengi husababishwa  na watu, kumkasirikia mtu aliyekusaliti, aliyekufilisi, anayekuroga ni  adhabu nyingine kubwa unayojipa mwenyewe, hivyo ili ufanikiwe kuondokana  na msongo wa mawazo ni vema ukawa mtu wa kusamehe na kutokuwa na hasira  na watu wengine ambao unadhani ndiyo chanzo cha tatizo lako.
NANE:  Unapokuwa na mawazo yanayoumiza na baadaye ukafanikiwa kuyaacha  usikubali kuyarudia tena, lakini watu wengi wanaoumizwa na mambo fulani  huwa hodari sana kuyatunza akilini mwao na kuyarejea kila mara, jambo  ambalo huwafanya waumizwe na mawazo hayo kwa muda mrefu bila kupumzika.  Yametokea, yamepita achana nayo usikubali akili yako iyarejee tena.
TISA:  Ikiwa umekuwa na mawazo ya kuumiza kwa muda mrefu, kwa sababu umefeli  mtihani au umeshindwa kufanya jambo fulani, mtu kakuudhi, hebu badili  mawazo hayo ya kushindwa na ufikirie kushinda katika siku za usoni.
Kwa  mfano kama hujazaa mtoto na ungependa kuwa naye, onja furaha hiyo kwa  kusema mwaka ujao utampata mtoto. Hatua hii itakusaidia kuitumikiwa  furaha hata kama katika hali ya kawaida hujaipata na hivyo kusogeza  mafanikio yako karibu zaidi.
KUMI: Yapo baadhi ya mambo ya  kuhuzunisha ambayo hutukumba bila kutarajia na hivyo kutuletea mawazo.  Njia pekee ya kuyaepuka mawazo ya aina hii ni pamoja na kukubali tukio  husika.
Wengi wetu tunapofiwa kwa mfano huwa hatukubali kuamini  kilichotokea, matokeo yake ni kuumia kwa muda mrefu. Unapokuwa na  tatizo, kwanza likubali kuwa limekupata kisha chukua hatuza za kufaa  kulikabili.
KUMI NA MOJA: Msongo wa mawazo unapokuvamia unatakiwa  wakati mwingine uchukue hatua za kujipumzisha sehemu tulivu, likiwepo  suala la kulala kama inawezekana. Hatua hii itasaidia kuupumzisha mwili  na akili kiasi cha kuufanya upate nguvu ya kukabiliana na tatizo.
Hushauriwi  kuchukua hatua unapokuwa na msongo mkali wa mawazo. Kama mtu amekuudhi,  achana naye nenda kajipumzishe, kesho utajikuta umepata nguvu ya  kumpuuza na kuachana naye kabisa.
KUMI NA MBILI: Wakati mwingine  kujua sababu zilizoleta tatizo ni muhimu na kwamba hupunguza msongo wa  mawazo. Hivyo unapokuwa na jambo ambalo linaikera akili yako, jaribu  kutafuta chanzo chake, inawezekana taarifa za mkeo kukusaliti  zinazokuvuruga si sahihi, ukiupata ukweli hasa, unaweza kubadili mawazo  yako na kupata nafuu ya maumivu.
KUMI NA TATU: Watu wengi  wanapopata matatizo ambayo huwatumbukiza katika mawazo mabaya huwa  hawako tayari kulipa gharama za kuyamaliza, matokeo yake hubaki  wakihuzunika. Kwa mfano mtu anaweza kuwa anadaiwa, mdai wake akamfuata  na kumtolea lugha za matusi, jambo la ajabu mdaiwa badala ya kujituma  kuhakikisha analipa deni ili ajikomboe anabaki kuhuzunikia matusi.  Unapokuwa na tatizo jitume kulimaliza kwa gharama yoyote ili uwe huru,  usikae kulia tu bila kupata ufumbuzi wa tatizo.
KUMI NA NNE: Njia  nyingine ya kuondokana na mawazo mabaya ni kuyakataa, kwa kufanya kitu  kingine ambacho kitakufanya usiwaze matatizo. Tatizo linalowakabili watu  mpaka wanashindwa kuyaondoa mawazo mabaya ni kutokuwa na vitu vingine  vya kufanya au kufikiri. Msomaji wangu unapojikuta umezama kwenye mawazo  yanayoumiza, bila kuchelewa chukua hatua za kuyakataa kwa kuingiza vitu  vingine akilini na kuanza kuviwaza, fanya kazi, soma vitabu fanya  mazoezi. Epuka pia upweke.
KUMI NA TANO: Tabia ya kukuza mambo  kupitia mawazo yetu ndiyo huchangia sana kuwa na mawazo ya kuumiza kwa  muda mrefu, inashauriwa kuwa mtu akipatwa na tatizo asilikuze kiasi cha  kuliona ni kubwa, asilostahili kulipata na kulifanya kuwa la tofauti  kwenye mawazo yake.
Ifahamike kuwa hakuna jambo baya kwa asili,  ukiwepo ubaya ni mawazo ya mtu mwenyewe. Dunia ni kioo, ukicheka nayo  itacheka ukinuna itanuna. Kwa maana hiyo ukiliwaza tatizo kwa ukubwa  litakuwa kubwa, ukilipunguza katika mawazo na kuliona ni la kawaida nalo  litakuwa hivyo.
Jambo la mwisho katika somo hili tunalipata kutoka  kwa Sir John Templeton ambaye alikuwa na kawaida ya kuwauliza watu ‘what  the definition of wealth?’ (Nini maana ya mafanikio ?) ambapo mwenyewe  alikuwa anawajibu ‘Live with an attitude of gratitude’ (Ishi katika  mtazamo wenye shukrani”.
Kwa kuhitimisha ili mtu aweze kuondokana na mawazo yenye kuumiza ni lazima awe mwenye kupokea kila jambo
Saturday, March 17, 2012
Hatua 15 za kuondoa mawazo yanayoumiza II
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment