Mateso na shida ulizopitia zisikurudishe nyuma, usikate tamaa  kabisa. Mwandishi mmoja  wa vitabu vya saikolojia, Willie Jolley aliwahi  kuandika katika kitabu chake cha It Only Takes A minute to Change your  Life kuwa; ‘Winners never quit and Quitters never win!’ (Washindi kamwe  hawakati tamaa na wakata tamaa kamwe hawashindi!). Maneno yao ya  kukuvunja moyo yageuze kuwa kuni za kuchochea moto wako wa mafanikio,  ili siku moja uje uwathibitishie kuwa wewe ni mshindi.
Kaa mbali  na marafiki wanaokatisha tamaa katika maisha. Fanya kazi kwa nguvu,  kuwa mbunifu, usiwe mtu wa kulalamika hovyo, chunga matumizi ya muda na  fedha, heshimu kila mtu aliyeko mbele yako, epuka kujikweza.
Kila siku endelea kujifunza vitu vipya.
Achana  na starehe ambazo hazina maana kabisa, jutia umasikini ulionao kwa  sasa, jiwekee mikakati muhimu ambayo itakuvusha. Kuanguka maishani ni  jambo la kawaida sana hasa katika safari hii ya kutafuta mafanikio.
Ngoja  nikupe mfano mmoja, Rais wa 16 wa Marekani, Abraham Lincoln alishindwa  mara nyingi mno kabla ya kuwa rais! Aliwahi kugombea ubunge akashindwa,  aliwahi kuanzisha biashara mbalimbali lakini alishindwa. Lakini baadaye  akashinda urais, hii ni baada ya kusota kwa muda mrefu sana.
Pamoja  na kushinda urais huo, bado alikutana na changamoto ya kudharaulika  lakini mwandishi mmoja aliandika makala kwenye gazeti ambayo ilisomeka;  ‘This is the most powerful president in the United States of America’  (Huyu ndiye rais mwenye nguvu kuliko wote katika nchi ya Marekani) ni  maneno hayo ndiyo yalibadili kabisa muonekano na fikra za rais huyo  ambaye baada ya kuamini maandishi hayo akapewa tuzo ya kuwa rais bora.  Na leo hii utawala wake unakumbukwa kuwa miongoni mwa tawala bora  Marekani na duniani kwa ujumla.
Hivyo basi ni lazima kuwepo maadui wakati wa kusaka mafanikio ambao watakusaidia kuchochea nguvu yako ya kutafuta maendeleo.
Kuwa  tayari kujitoa hata katika hatari ambazo ni mbaya zaidi. Mafanikio  yanapatikana palipo na hatari (Success dwell on the edge).
Mbinu  nyingine ya kupata mafanikio ni pamoja na kutumia muda mwingi ukiwa  kimya ukitafakari mambo, kwani akili iliyotulia ndiyo hupata nafasi  nzuri ya kubuni mambo ya muhimu. Kuwa mkimya muda mwingi, achana na  maneno mengi kwani hayakusaidii kwa lolote zaidi ya kukuchosha kwani  unatumia nguvu nyingi mno katika kuongea. Rafiki yangu mmoja aliniambia   ‘Silence means a lot’ akimaanisha kuwa ukimya humaanisha mengi. Wewe  kuwa kimya, fanya mambo kwa vitendo.
Jambo lingine la muhimu  kuzingatia ni kuachana kabisa na tabia ya kufanya jambo kwa ajili ya  kutafuta sifa. Achana na sifa ambazo hazikusaidii kwa lolote. Fanya  mambo kulingana na jinsi moyo wako unavyokuelekeza kwa manufaa yako na  si kwa ajili ya kusifiwa. Wengi wafanyao hivyo huwa hawafanikiwi kamwe.  Dunia ya sasa si ya kutaka sifa na maneno mengi. Hii ni dunia ya vitendo  na ustaarabu. Epuka kubishana na mtu yeyote kwa jambo lolote.
Achana  na ugomvi wa aina yoyote, fanya kazi kwa nguvu na ubunifu wa hali ya  juu. Jambo lingine muhimu ni kujifunza kusaidia watu. Pendelea sana  kusaidia watu kwa namna yoyote ambayo unaweza, na ukimsaidia mtu  hakikisha hakuna mtu anayejua.
Usitoe msaada kwa kujitangaza kwa  watu. Kwa kufanya hivyo msaada wako hautakuwa na maana kwani hauna  baraka za Mungu. Nikiwa naelekea mwisho wa makala haya, naomba  nikukumbushe jambo muhimu sana kuwa maisha ni jinsi unavyoishi.
Mwamuzi  wa hatima ya maisha yako ya kesho ni wewe mwenyewe na si mtu mwingine.  Ukiamua kufanikiwa na ukajiwekea dhamana, basi ni lazima ufanikiwe. Pia  kumbuka kuwa mafanikio ya kesho yanajengwa leo kwani mafanikio ya leo  yalijengwa jana. Kila kitu kinawezekana hapa chini ya jua endapo tu  utaamua kwa dhati. Naomba nikutakie mafanikio mema kwa mwaka huu wa 2012  ambapo naamini kama utayazingatia haya basi mafanikio kwako ni lazima.  Mwisho
Thursday, March 15, 2012
Anza Mwaka na Mawazo Mapya III
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment