Nini  sababu ya kuandika mada hii? Inatokana na kupata swali la mwanamke  ambaye aliingia katika gogoro na mumewe kutokana na kukutwa katika  mazingira yasiyo salama. 
 
Kutokana na maelezo yake kuna kaka  mmoja alikuwa akimtaka kimapenzi japo alijua ni mke wa mtu, alimkatalia  lakini kaka yule hakuchoka kumfuatilia.
  
Siku moja wakati  anatoka dukani alikutana na kaka yule na kumsimamisha, baada ya kusimama  aliendelea kumwagia sera kwa muda huku yule dada akijitahidi kumkatalia  kwa bahati mbaya mumewe aliwaona.
Alimuuliza juu ya yule  mwanaume, naye akajitetea kuwa alikuwa akimtongoza lakini alimkatalia,  mumewe hakumuelewa na kusema yule ni ‘mtu wake’.
 
Aliomba msaada wa kuokoa ndoa yake, nimlimpa ushauri uliomsaidia kurudisha amani katika ndoa yake.
 
Lakini  matatizo hayo yamewakuta wanawake wengi kukutwa na wanaume wao sehemu  zisizo salama japo hawakuwa tayari kusaliti ndoa zao.
KUSUDI LA  MADA HII NI NINI? Nina imani ulisoma mada ya wiki jana kuhusu wivu ambao  niliuelezea kwa upana sana, lakini baadhi ya mazingira hayafai kwa mke  au mume wa mtu kusimama.
 
Sawa mtu anakutongoza lakini humtaki  mnatumia zaidi ya robo saa kuzungumza na mtu ambaye si sahihi kwako  unazungumza nini?  Kama umeolewa ukisha jibu ‘nimeolewa’ lakini akazidi  kukusumbua mwambie ‘sitaki’,  naneno yasiyo chukua hata sekunde mbili.
 
Unapokuwa  ndani ya mamlaka ya mtu unatakiwa kujiheshimu na kuyaepuka mazingira  yote yanayoweza kutoa tafsiri mbaya kwa watu wa pembeni.
 
Umetongozwa  mke wa mtu ufanye nini? Kwa vile mke wa mtu huwa hana muhuri, si wote  wanaotembea na pete, kama mwanaume amekutongoza na kumueleza kuwa  umeolewa na bado anakufuata unachotakiwa kuyafanya ni haya:
 
Moja,  usikubali kusimama atakapo kusimamisha, huwezi kukataa salamu yake ila  jiepushe kupokea neno litakalofuata lisilokuwa salama kwako.
Japo  wapo wanawake wenye msimamo, lakini baadhi ya maneno ya wanaume kama  utakubali kuyasikiliza yana nguvu ya kuivunja ngome ya moyo wako na  kufikia hatua ya kumsaliti mumeo.
 
Pili, Ishi mazingira salama.
Mazingira  salama ni yapi? Kujiheshimu, mwanamke anayejiheshimu humuweka mbali na  wanaume wakwale tofauti na mwanamke asiyejiheshimu ambao hawana kinga  yoyote na kumfanya mwanaume kusema lolote. 
Tatu, jiepushe na mazoea ya kuvuka mipaka na wanaume ambayo huwapa nafasi wakwale kuingiza mambo yako.
 
Nne,  unapomweleza mwanaume umeolewa onyesha kweli unaiheshimu ndoa yako na  si kusema huku unacheka kuonyesha maneno yako ni ya mdomoni wala si  moyoni.
 
Tano, usimpe nafasi mwanaume anayekutongoza akushambulie kwa maneno na wewe umesimama unamsikiliza lazima atakushinda.
Sita,  lazima ujue thamani yako unapokuwa mke wa mtu kwa kuvaa nguo za  heshima, kuwa mbali na wanaume wenye mazoea yaliyovuka mipaka kama  kuzungumza maneno yaliyokosa staha pia hata kukugusa sehemu nyeti  kujifanya wanakutania.
  
Saba, angalia mazingira ya kusimama na mwanaume na yasizidi dakika mbili labda awe na shida kubwa inayoitaji msaada wako.
Saturday, March 17, 2012
Jinsi "mke wa mtu" Anaweza Kujiepusha na Mazingira Hatarishi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment