Saturday, March 17, 2012

Jinsi "mke wa mtu" Anaweza Kujiepusha na Mazingira Hatarishi

Nini sababu ya kuandika mada hii? Inatokana na kupata swali la mwanamke ambaye aliingia katika gogoro na mumewe kutokana na kukutwa katika mazingira yasiyo salama.

Kutokana na maelezo yake kuna kaka mmoja alikuwa akimtaka kimapenzi japo alijua ni mke wa mtu, alimkatalia lakini kaka yule hakuchoka kumfuatilia.

Siku moja wakati anatoka dukani alikutana na kaka yule na kumsimamisha, baada ya kusimama aliendelea kumwagia sera kwa muda huku yule dada akijitahidi kumkatalia kwa bahati mbaya mumewe aliwaona.

Alimuuliza juu ya yule mwanaume, naye akajitetea kuwa alikuwa akimtongoza lakini alimkatalia, mumewe hakumuelewa na kusema yule ni ‘mtu wake’.

Aliomba msaada wa kuokoa ndoa yake, nimlimpa ushauri uliomsaidia kurudisha amani katika ndoa yake.

Lakini matatizo hayo yamewakuta wanawake wengi kukutwa na wanaume wao sehemu zisizo salama japo hawakuwa tayari kusaliti ndoa zao.

KUSUDI LA MADA HII NI NINI? Nina imani ulisoma mada ya wiki jana kuhusu wivu ambao niliuelezea kwa upana sana, lakini baadhi ya mazingira hayafai kwa mke au mume wa mtu kusimama.

Sawa mtu anakutongoza lakini humtaki mnatumia zaidi ya robo saa kuzungumza na mtu ambaye si sahihi kwako unazungumza nini? Kama umeolewa ukisha jibu ‘nimeolewa’ lakini akazidi kukusumbua mwambie ‘sitaki’, naneno yasiyo chukua hata sekunde mbili.

Unapokuwa ndani ya mamlaka ya mtu unatakiwa kujiheshimu na kuyaepuka mazingira yote yanayoweza kutoa tafsiri mbaya kwa watu wa pembeni.

Umetongozwa mke wa mtu ufanye nini? Kwa vile mke wa mtu huwa hana muhuri, si wote wanaotembea na pete, kama mwanaume amekutongoza na kumueleza kuwa umeolewa na bado anakufuata unachotakiwa kuyafanya ni haya:

Moja, usikubali kusimama atakapo kusimamisha, huwezi kukataa salamu yake ila jiepushe kupokea neno litakalofuata lisilokuwa salama kwako.

Japo wapo wanawake wenye msimamo, lakini baadhi ya maneno ya wanaume kama utakubali kuyasikiliza yana nguvu ya kuivunja ngome ya moyo wako na kufikia hatua ya kumsaliti mumeo.

Pili, Ishi mazingira salama.

Mazingira salama ni yapi? Kujiheshimu, mwanamke anayejiheshimu humuweka mbali na wanaume wakwale tofauti na mwanamke asiyejiheshimu ambao hawana kinga yoyote na kumfanya mwanaume kusema lolote.

Tatu, jiepushe na mazoea ya kuvuka mipaka na wanaume ambayo huwapa nafasi wakwale kuingiza mambo yako.

Nne, unapomweleza mwanaume umeolewa onyesha kweli unaiheshimu ndoa yako na si kusema huku unacheka kuonyesha maneno yako ni ya mdomoni wala si moyoni.

Tano, usimpe nafasi mwanaume anayekutongoza akushambulie kwa maneno na wewe umesimama unamsikiliza lazima atakushinda.

Sita, lazima ujue thamani yako unapokuwa mke wa mtu kwa kuvaa nguo za heshima, kuwa mbali na wanaume wenye mazoea yaliyovuka mipaka kama kuzungumza maneno yaliyokosa staha pia hata kukugusa sehemu nyeti kujifanya wanakutania.

Saba, angalia mazingira ya kusimama na mwanaume na yasizidi dakika mbili labda awe na shida kubwa inayoitaji msaada wako.

Related Posts by Categories



No comments:

Post a Comment