WIKI hii kwenye makala haya ya Jitambue tutajifunza mambo muhimu  ambayo yatasaidia kutuwezesha kuishi kwa mafanikio na furaha zaidi.  Ombi langu kwako msomaji ni kutafakari kwa kina dondoo zifuatazo ambazo  nitazifasiri kwa ufupi sana.
Usiwe mtumwa wa umakini  sana – Watu wengi hawafanikiwi kwa sababu ni watumwa wa umakini,  hawafanyi au hawajaribu kufanya mambo ambayo akili zao zinawasiwasi  nayo. Usiwe mtumwa wa usahihi, dunia haiwasifii wale wanaofanya mambo  kikamilifu, bali huwasifia wale ambao hujitahidi kufanya chochote na  kufanikiwa.
Usitake kujilinganisha na wengine – Fahamu kwamba katika kila ulifanyalo, mtu unayeshindana naye ni wewe mwenyewe.
Usifikirie  sana mambo yaliyopita au kuhangaikia sana mambo ya siku zijazo –   Fikiria na kujishughulisha na mambo yaliyopo sasa.  Wakati huu ndiyo wa  maisha yako yanayofahamika.  Usiikose fursa hii.
Acha kulalamika – Dawa ya kulalamika ni kufanya kitu fulani ili kulitatua tatizo linalokukabili.
Usiwe na moyo wa kuendeleza kinyongo – Kuendeleza moyo wa kinyongo ni kupoteza muda ambao ungekufanya uwe na furaha.
Usiwe  mtu wa kusubiri kufanya jambo fulani baadaye – Kile ambacho hutakianza  leo ni dhahiri hautakimaliza kesho.  Maarifa na busara ni vya bure iwapo  mtu atachukua hatua ya kufanya vitendo vinavyotakiwa.
Acha  kusema uongo – Katika kila hali ukweli baadaye hujitokeza.  Hivyo,  inabidi uwe mkweli katika vitendo vyako, la sivyo hatimaye vitendo hivyo  vitakuumbua.
Acha tabia ya kukwepa kufanya makosa – Kosa pekee  ambalo litakuumiza ni kuamua kutofanya chochote kwa vile unaogopa mno  kufanya kosa. Siku zote tunajifunza kutokana na makosa.
Acha kusema,  “siwezi” – Kama Henry Ford alivyowahi kusema, “Ukifikiri unaweza au  ukifikiri huwezi, bado uko sahihi.” Ukisema huwezi hutaweza na ukisema  naweza utaweza.
Acha kujiona  unajua kila kitu na huna shida na  watu wengine – Wakati mwingine maisha ya mwanadamu yanategemea mawazo ya  wenzake, kuwa tayari kujifunza kutoka kwa wengine.
Acha kufikiri  kwamba  hauko tayari kufanya jambo fulani – Kuwaza mafanikio ni  kujiumiza, mara kadhaa unapofikiria kufanya jambo fulani utaona kama  haliwezekani na hali ya kufadhaika hutokea, jiamini usiwe mtu wa kukata  tamaa.
Acha kujiwekea malengo madogo – Watu wengi hujiwekea  malengo madogo kwa vile huwa wanaogopa kushindwa kuyatekeleza.  Ukweli  ni kwamba, kujiwekea malengo madogo ndiko kunakowafanya washindwe katika  maisha. Weka malengo makubwa ya mafanikio ili ukipata kidogo usiwe  kwenye fungu la kukosa.
Usitake kila kitu ukifanye wewe – Wewe ni  sehemu ya watu wengine ambao unaishi nao kwa muda mrefu zaidi.   Mkifanya kazi pamoja mtakuwa na nguvu zaidi kuliko ambavyo ungefanya  jambo fulani pake yako.
Acha kununua vitu ambavyo huvihitaji –  Hakikisha unazitumia fedha zako kwa busara na usikubali zikakutawala.   Usitake kuzitumia kwa mambo ya kuwafurahisha wengine.  Usitake kuwa na  maisha ya kujipumbaza kwamba utajiri hupimwa kwa vitu ambavyo mtu  anavyo.
Acha kuwalaumu watu wengine kwa matatizo yako – Kiwango  cha kutimiza ndoto maishani mwako kinategemea jinsi unavyoyashughulikia  maisha yako.  Ukianza kuwalaumu wengine kwa yale yanayokutokea, utakuwa  unajivua majukumu, kwani majukumu ya kutatua matatizo yako unakuwa  umewapa watu wengine.
Itaendelea wiki ijayo.
Thursday, March 15, 2012
Mambo ya muhimu ya kuzingatia kwenye maisha ya kila siku I
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment