Utafiti wa kisaikolojia  unaonesha kuwa, watu wengi sana wameweza kutimiza malengo waliyojiwekea  maishani,lakini bado hawajafanikiwa hata kidogo japo wana kila kitu  walichokihitaji katika maisha yao hapa duniani!Wapo waliokuwa na malengo  ya kuwa madaktari,wanasheria,waalimu,waandishi wa habari na kila aina  ya maisha mazuri ikiwemo kumiliki magari ya kifahari, majumba na wake  wazuri lakini bado wanalia kwani hawajafanikiwa.
Hapa chini nitaainisha kwa ufupi maana za haya maneno mawili na jinsi ya kuyatofautisha.
KUTIMIZA LENGO:
Hapa ndipo kwenye mkanganyiko mkubwa sana, kwani watu wengi huishia hapa na wakifikiri kuwa tayari wameshafanikiwa maishani.
Kutimiza  lengo ni kitendo cha kufikia yale uliyokuwa unayatamani kwa muda mrefu,  yaani kupata kile ulichokihitaji maishani. Mfano labda ulikuwa na ndoto  ya kuwa mhasibu, ukasoma kwa nguvu na bidii zote na hatimaye ukafikia  kuwa mhasibu. Basi hapo unakuwa umetimiza lengo na kufanikiwa.
Mwandishi  mmoja wa mambo ya saikolojia, Halord Sherman aliwahi kuandika katika  kitabu chake cha The New TNT Miraculous  Power within You kuwa, Getting  what you ever wanted in Life, doesn’t indicate success’ akimaanisha kuwa  kupata kila kitu ulichokihitaji maishani, haiashirii mafanikio’ na  kwamba unaweza kutimiza kile unachokitaka lakini bado ukawa hujafanikiwa  maana hauna furaha nacho! Kufanikiwa ni kufurahia ulichokifikia.
KUFANIKIWA:
Hiki  ni kitendo cha kufurahia kile ulichokipata. Ni kweli kabisa ulitaka  kuwa mwandishi wa habari sawa, lakini je, unafurahia uandishi wako wa  habari? Ni kweli kabisa ulikuwa na ndoto na malengo ya kuwa mbunge,  daktari, mkulima nk. Swali linabaki palepale kuwa una furaha na  unachokifanya?
Nadhani sasa msomaji utakuwa umepata mwanga katika kutofautisha maneno haya mawili kati ya kutimiza lengo na kufanikiwa.
Hivyo  basi kwa pamoja tumeweza kuona kuwa, kutimiza lengo ni kufikia au  kupata kile ulichokuwa unakihitaji na kufanikiwa ni kuwa na furaha na  ulichokipata.
Kwa hiyo mtu anaweza kufikia lengo lake lakini bado akawa hajafanikiwa kwa sababu hafurahii alichokipata.
Chukulia  mfano kuwa, ulikuwa na hamu kubwa sana ya kununua gari na hilo likawa  ndilo lengo lako. Baada ya mwaka mmoja ukanunua gari kweli. Lakini kila  siku gari hilo linaharibika, halitunzi mafuta kila siku uko gereji. Je,  utakuwa umefanikiwa kweli? Hapana, utakuwa umetimiza lengo la kununua  gari  lakini bado hujafanikiwa.
Mfano mwingine ni huu, wakati  ukiwa kijana, ulikuwa na malengo ya kupata mume au mke bora, na ulipokua  kweli ukapata mke/mume mzuri na familia bora. Kweli, baada ya miaka  kadhaa ukapata mume/mke mzuri kama ulivyokuwa umelenga.
Lakini  baada ya kuingia kwenye ndoa kila siku inakuwa ni ugomvi, malumbano na  migogoro isiyoisha.Je, unakuwa umefanikiwa? Au umetimiza lengo la kuwa  na mke/mume bora?
Jibu ni wazi kuwa unakuwa umetimiza lengo lakini unakuwa hujafanikiwa.
Jambo  la msingi ambalo nataka kulisisitiza hapa ni kuwa, ni lazima umakini  utumike katika kujiwekea malengo maishani. Jiwekee malengo ambayo  ukiyatimiza basi ufurahie kuyafanya.
KATIKA maisha, ni bora ukajiwekea utaratibu wa kumtegemea Mungu maana  yeye ndiyo kila kitu katika maisha yetu. Achana na ujanja wote wa  kibinadamu.
Kuna msemo mmoja ambao aliwahi kuuongea King Martin Luther katika moja ya hotuba zake ambao unasema:
‘Don’t battle a war that  you know you cant win!’ yaani akimaanisha usipigane vita ambayo unajua kabisa huwezi kushinda’.
Kwa  nini nimetoa mfano huu, watu wengi sana wamekuwa wakifanya mambo ambayo  hayawasaidii kupata maendeleo maishani mwao, na wanafanya hivyo kwa  sababau tu fulani anafanya. Hayo siyo maisha.
Shida ambazo  unazipitia kwa sasa, usizichukie na badala yake sasa zigeuze shida hizo  kuwa kuni za kuchochea nguvu zako za kuelekea maishani. Usipende sana  kujihukumu kwa makosa ambayo umeyafanya huko nyuma kwani hayawezi  kufutika kwa kujilaumu na badala yake sasa anza upya kwa kufanya kazi  kwa bidii huku ukibadilika siku hadi siku. Dada yangu mmoja ambaye ni  mfanyakazi mwenzangu naomba nimtaje kwa jina moja la  Naila  aliwahi  kuniambia kuwa:
“No one can go back and change a bad beginning.  But any one can start now and create a successful ending. Every  successful person has painful story! Every painful story has a  successful ending.
Accept the pain and get ready for success. Have a good start!
Ni maneno yanayotia nuru mpya maishani. Dada huyu alimaanisha:
“Hakuna mtu anayeweza kubadilisha mwanzo mbaya. Lakini mtu anaweza kuanza na kutengeneza mwisho wenye mafanikio.
Kila  mtu mwenye mafanikio ana historia yenye maumivu! Kila historia yenye  maumivu ina mwisho wenye mafanikio. Kubali maumivu na uwe tayari kwa  mafanikio. Nakutakia mwanzo mpya!”
Hata wewe msomaji wangu, endelea kupambana na maisha. Usikubali mtu yeyote akuvunje moyo.
Unapoanza  safari ya kutafuta mafanikio, vitainuka vikwazo vingi mno. Watu  watakuambia maneno ya kukatisha tamaa, watasema huwezi kwa sababu  hukusoma, familia yako masikini na mengine mengi ya kuvunja moyo na  kuondoa matumaini.
 Jambo moja la kuzingatia ni kuwa, hakuna binadamu  anayeweza kukuamulia maisha yako yawe vipi. Thamani yako ni kubwa sana  na malengo uliyojiwekea ni lazima uyatimize na hatimaye kufanikiwa.
Saturday, March 17, 2012
Tofauti kati ya kutimiza lengo na kufanikiwa!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment